Uchunguzi uliofanywa na wataalamu wa silaha wa Amnesty International umebaini kuwa, bomu lililotumiwa na Saudia kuua raia hao lina sifa za mabomu ya Marekani yanayorushwa na ndege na kuongozwa kwa leza.
Ripoti hiyo imesisitiza kuwa, mashambulizi yanayofanywa na Saudi Arabia na washirika wake dhidi ya Yemen yanaendelea kuwa sababu kuuya mauaji ya raia hususan watoto wadogo nchini Yemen.
Matokeo hayo ya utafiti wa Amnesty International yametolewa baada ya Umoja wa Ulaya kuwasilisha muswada katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa ukitaka kufanyike uchunguzi kuhusu ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanyika nchini Yemen.
Shambulizi la ndege za Saudi Arabia lililofanyika tarehe 25 mwezi uliopita wa Agosti katika makazi ya raia mjini Sana'a liliua raia 16 wakiwemo wazazi wawili na mtoto Buthaina na ndugu zake watano. Alipoulizwa anataka kufanya nini, Buthaina mwenye umri wa miaka 5 ambaye amebakia peke yake kati ya watu wote wa familia yake, alisema anataka kurudi nyumbani na kucheza na ndugu zake.
Picha zilizooneshwa na vyombo vya habari za mtoto huyo ndogo wa Yemen aliyebakia peke yake baada ya familia yake yote kuuawa na ndege za Saudi Arabia zimewasikitisha sana walimwengu. Buthaina aliyejeruhiwa katika shambulizi hilo amepoteza jicho lake moja.
Takwimu zainaonesha kuwa katika hujuma za kinyama za Saudia dhidi ya Yemen Machi 2015, watu karibu 13,000 wameuawa wengi wao wakiwa ni raia hasa watoto na wanawake.