TEHRAN (IQNA)- Makumi ya raia, aghalabu wakiwa wasichana wa shule waliuawa shahidi Jumamosi katika hujuma ya kigaidi dhidi ya shule ya Sayyid al Shuhadaa katika mtaa wa Dasht-e-Barchiwenye Waislamu wengi wa madhehebu ya Shia katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul.
Rais wa Afghanistan Ashraf Ghani amesema kundi la Taliban limehusika na hujuma hiyo. Hatahivyo kundi hilo halijatangaza kuhusika na baadhi ya duru za habari zinasema kundi la kigaidi la ISIS au Daesh ndilo ambalo limehusika na jinai hiyo.