Sayyed Musaad, Naibu Mkuu wa Idara ya Waqfu mjini Cairo ameyasema hayo Jumanne wakati wa kuwattunuku zawadi washindi wa mashindano ya Qur'ani.
Mashindano hayo yaliandaliwa katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa ajili ya waliohifadhi Qur'ani kaitka taasisi za Qur'ani zisizo za kiserikali.
Aliongeza kuwa, wazazi wanapaswa kujitahidi kuwapa watoto wao mafunzo sahihi ya Qur'ani Tukufu ili kuwawezesha kujizuia kutumbukia katika misimamo mikali na utumiaji mabavu.
Sayyed Musaad amesisitiza kuwa, Qur'ani Tukufu inamfunza mwanadamu namna ya kuishi kwa kutafakari kuhusu mafundisho ya kitabu hicho kitukufu lengo likiwa ni kuletta usalama na amani katika jamii.
Kila mwaka katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani jamii za Waislamu kote duniani huandaa mashindano ya Qur'ani Tukufu.