Katika taarifa siku ya Jumanne, CAIR imesema kumeshuhudiwa ongezeko la hujuma au vitendo vinavyochochewa na chuki dhidi ya Waislamu tokea Donald Trump ashinde uchaguzi wa rais Marekani mwaka 2016.
Kwa mujibu wa CAIR kutokana na kuwa katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani idadi ya Waislamu wanaojumuika katikamisikiti au vitu vya Kiislamu huongezeka, kuna uwezakano mkubwa kuwa watu wenye chuki dhidi ya Waislamu wakawashambulia Waislamu.
Kwa msingio huo Waislamu wametakiwa kuimarisha usalama katika misikiti na vituo vya Kiislamu au sehemu yoyote ile wanayojumuika kwa ajili ya ibada.
Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unatazamiwa kuanza Mei 15 nchini Marekani na kumalizika Juni 14.
3465777