IQNA-Mamlaka ya Huduma za Msikiti Mtukufu wa Makka na Msikiti wa Mtume (SAW) jijini Madina imetangaza ongezeko kubwa la wageni katika mwezi wa Jumada Al-Awwal 1447 Hijria Qamaria, ambapo jumla ya watu milioni 66.6 walitembelea misikiti hiyo miwili mitukufu. Idadi hii imeongezeka kwa zaidi ya milioni 12 ikilinganishwa na kipindi kilichopita, kwa mujibu wa Shirika la Habari la Saudi.
19:19 , 2025 Nov 28